Wasiliana nasi | FAQ | Mails | Malalamiko |

Tanga Regional Referral Hospital
(Bombo Hospital)

Mpango Binafsi wa kujifungua Salama

Posted on: October 18th, 2019

 ANDAA,ZUNGUMZA NA MWENZI WAKO,JAZA MPANGO

  • Fahamu tarehe ya kujifungua.
  • Fahamu na uhakikishe kituo cha kutolea huduma za afya au hospitali utakapojifungulia.
  • Fanya mpango wa usafiri wa kukufikisha mapema kwenye kituo cha kutolea huduma za afya utakapojifungulia.
  • Nani atakaye kusindikiza kwenye kituo cha kutolea huduma za afya mapema ili ujifungulie huko.
  • Tayarisha mfuko utakapoweka nguo za mtoto na mahitaji yote wakati ukiwa katika kituo cha kutolea huduma za afya.
  • Nani utakayemwachia nyumba utakapoenda kujifungua?
  •  Jadili na mwenza wako na mtoa huduma iwapo unataka kubadili mpango

ORODHA YA HUDUMA KWA MAMA MJAMZITO UENDAPO KLINIKI

  • Vipimo vya kuzingatia kila uendapo kliniki
  • Kipimo cha presha ya damu
  • Kipimo cha kiwango cha damu
  • Kipimo cha mkojo
  • Mtoto anavyoendelea kukua tumboni
  • Vipimo vinavyofanyika angalau mara moja wakati wa ujauzito
  • Kipimo cha kundi la damu
  • Kipimo cha magonjwa ya zinaa mfano Kaswende
  • Kipimo cha Virusi Vya Ukimwi kwako na mwenza wako(kawaida mara mbili)
  • Hakikisha unapata vitu hivi
  • Chandarua chenye dawa( viatilifu)
  • Chanjo za pepopunda
  • Vidonge vya kuongeza damu(Tumia kila siku wakati wa ujauzito na endelea kutumia vidonge vya kuongeza damu mpaka miezi mitatu baada ya kujifungua)
  • Dawa za minyoo(Tumia mara moja baada ya miezi mitatu ya ujauzito
  • Vidonge vya SP kuanzia wiki ya 14 ya ujauzito na kila unapohudhuria kituo cha kutolea huduma za afya.

DALILI ZA HATARI KABLA YA KUJIFUNGUA/WAKATI WA KUJIFUNGUA/BAADA YA KUJIFUNGUA

  • Uonapo dalili hizi nenda kituo cha kutolea huduma za afya mara moja!!!
  • Kutoka damu ukeni
  • Kuumwa sana na kichwa na kuona maluweluwe/kushindwa kuona
  • Kupoteza fahamu au mtukutiko mwili/kifafa cha mimba
  • Kuchoka haraka ,kupumua kwa shida
  • Homa
  • Mtoto kuacha au kupunguza kucheza tumboni.
  • Dalili za ishara za uchungu wa kujifungua
  • Mkazo na kuachia kwa misuli ya mfuko wa uzazi unaoendelea kuongezeka na kusababisha  maumivu makali ya tumbo na kiuno hadi kujifungua.
  • Kutokwa mchozo ute wenye damu.

KUMBUKA: Kama unaishi mbali na kituo cha kutolea huduma za afya ,ni busara kuhamia kwa muda karibu na kituo hicho,kadiri siku ya kujifungua inavyokaribia.


Imeandaliwa na:

DOROTHY A LEMA

MRATIBU WA HUDUMA YA AFYA YA UZAZI NA MTOTO -TANGA